- Waninunia mie.....umekosa mwenyewe magoli ya penati utayaweza ya kona.......
- Japo chungu we meza tu....
- Kufika utafika hata kama ukitembea....
- Mola nipe jicho la tatu linijaze ufahamu....
- Aliyekuonjesha kaweke kambi kwake.....
- Eti kuku wa kuchora....hawiki, hatagi yai wala hadonoi.....
- Unaacha nyama nyumbani unaenda kula mishikaki baa....
- Umezoea cheko la nyundo hebu tupe la msumari sie nginjha nginjha....
- Uko busy airport unasubiri meli na hata passport hujabeba.......
- Umeumbwa u-kanga unataka u-kuku.....
- Uko busy kama unapiga deki bahari.....
- Japo chungu we meza tu......
- Donda la maskini hupona kwa umande.....
- Kobe hufika aendako hata akienda taratibu......
- Usijifanye unachagua wakati bado unachaguliwa......
- Hata tausi mrembo lakini haliwi nyama....
- Mbwa mzee hafundishwi sheria mpya.....
- Ingekuwa rahisi hata samaki angetafuta perfume......
- Aaahhh papai kubwa ka-apple kadogoo...bei ya apple sasa, papai halina maana....
- Uniniletea perege mie, hicho kidagaa....niletee yule papa ndio saizi yangu
- Hukushiba kwa tonge, utashiba kwa kulamba....
- Ukimuona kobe juu ya mti ujue kapandishwa......
- Madogo madogo yakupite na makubwa yakusakame....
- Huwezi kuwa mkwezi ukashindwa kusuka pakacha......
- Mchele kisoda, nazi sita.....
- Usipaki fuso kwenye gereji ya bajaji...
- Usipite kimyakimya uliza njia usije ukajigonga buree...
- Muwasho wa ulimi, haukunwi na kidole....
- Kama bahari.....ukiweka lindo kaskazini wenzio kusini wanavua....
- Mzoea punda, hapandi farasi.....
- Bora kandambili kuliko mdundo mbovu....
- Unavua samaki kwa mikono, utamaliza kesho.....
- Ukibipu tu, mi nakupigia.....
- Una maswali mengi, kwani we ni polisi.....
- Unaniongelesha kizungu, umenisomesha wewe......
- Mchuma janga, hula na wa kwao.....
- Zege halilali.....
- Ukimjua adui yako unamshinda kirahisi.....
- Unapanda basi la bagamoyo wakati unaenda ikwiriri.......
- Uko kama majani ya chai, hujulikani kama dawa ya ngiri au ya kichwa.......
- Ameshakuwa kuku wa kwenye jokofu, kapoteza radha..........
No comments:
Post a Comment