Nyoka Jamii ya Cobra |
SERIKALI imedhamiria
kumsaka nyoka mwenye umri wa miaka 209 aliyepo katika Msitu wa Akiba Minziro,
uliopo Wilaya ya Misenyi, mkoani Kagera. Lengo la kumsaka nyoka huyo ni
kutokana na ukongwe wake hivyo kuwa kivutio kikubwa duniani hasa katika sekta
ya utalii.
Mkurugenzi wa Misitu
na Nyuki nchini, Dkt. Felician Kilahama, aliyasema hayo juzi wakati akizungumza
na waandishi wa habari. Alisema nyoka huyo mwenye futi 47, atapatikana baada ya
mapito yake katika msitu huo kuonekana ila ni vigumu kuonekana hadharani kwa
sababu hupendelea kuishi mapangoni.
“Huyu nyoka lazima
tumfanyie mahesabu ya kumkamata kirahisi, umri wa miaka 209 sio mchezo, ameweza
kutambulika Baada ya kupima urefu wa mapito yake, pia kuna chatu na nyoka wenye
mapembe,” alisema Dkt. Kilahama.
Aliongeza kuwa, licha
ya nyoka kuhatarisha maisha ya watafiti lazima kufanyike uharaka wa kuupandisha
hadhi msitu huo uwe hifadhi ya Taifa ili kuboresha usimamizi wake.
“Kikao cha Kamati ya
Ushauri cha Mkoa Kagera (RCC), kilipitisha msitu huu upandishwe hadhi, nyoka
huyu ambaye ni aina ya Giant Forest Cobra, kichwa chake kina rangi nyekundu na
sehemu ya kiwiliwili rangi ya kijani.
“Alianza kufanyiwa
utafiti mwaka 2000 baada ya kupatikana kwa taarifa kutoka kwa wenyeji wa maeneo
hayo juu ya kuwepo kwa aina ya nyoka huyo katika msitu huu,” alisema.
Kutokana na hali hiyo,
uongozi wa Halmashauri ya Missenyi, kupitia Maofisa wa Misitu, mwaka 2010
walianza kuweka mitego ya sindano katika mapito anayotumia ili kuchukua damu
yake na kwenda kuipima vina saba ndipo ilibainika kuwa hadi kufikia mwaka huo,
alikuwa na miaka zaidi ya 207. Dkt. Kilahama alisema nyoka huyo atakuwa kivutio
muhimu mkoani hapa kama atapatikana licha ya kukabiliwa na tatizo la ukumbwa wa
msitu ambao hekta 25,000 kwani nyoka huyo amekuwa akihama mara kwa mara kwa
ajili ya mawindo.
Ofisa Misitu wilayani
hapa, Bw. Wilbard Bayona, alisema nyoka huyo ana uwezo wa kuishi siku 68 bila
kula chochote zaidi ya maji baada ya kumeza mnyama yeyote ambaye atamkamata
mawindoni.
Habari kutokana mitandao mbalimbali
No comments:
Post a Comment