Thursday, October 11, 2012

Uchumi wa Uingereza upo hatarini kuporomoka vibaya

David Cameron
Waziri Mkuu wa Uingereza

Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, ameonya kuwa Uingereza itaanguka kiuchumi na kuvuta mkia nyuma ya Brazil, China na India iwapo haitapunguza nakisi ya bajeti yake na kuwa ya ushindani zaidi.
Bw Cameron ameuambia mkutano mkuu wa kila mwaka wa chama chake cha Conservative kuwa Uingereza inaweza kukabiliana na changamoto hiyo kwa kuimarisha elimu yake, kupunguza matumizi katika ustawi wa jamii na kuausha ari miongoni mwa watu wake.
Ingawa imechukua muda mrefu kuliko ilivyotarajiwa kwa Uingereza kurekebisha uchumi wake urejee kwenye kukua tena, Cameron amesema nakisi ya taifa imepunguzwa kwa kiasi cha robo katika miaka miwili iliyopita.

No comments: