Maafisa kumi na wanne wa kiufundi wa Uganda waliokuwa katika ndege mbili za kivita iliyopotelea katika angaa la Kenya zikienda Somalia wameokolewa wakiwa hai.
Afisa wa uokoaji kutoka katika shirika la wanyapori nchini Kenya amesema kuwa watu hao waliokolewa kutokana na ndege zao kutoshika moto baada ya kuanguka huku wakipata maiti ya wanajeshi wawili kutoka kwenye ndege nyingine iliyoanguka na kushika moto.
Awali,msemaji wa jeshi la Kenya Bogita Ongeri alisema ndege mbili zilikuwa zimepatikana zikiwa zimeungua ila watu waliokuwemo ndani wanaokadiriwa kuwa kumi hatima yao ilikuwa bado haijafahamika.
Ndege zingine mbili ambazo pia zilianguka katika mlima huo zilipatikana jana na watu saba walikuwa katika ndege hiyo waliokolewa wakiwa hai.
No comments:
Post a Comment