Wednesday, September 12, 2012

Watu 240 wafariki kutika mkasa wa moto nchini Pakistan


Zaidi ya watu mia mbili arobaini wamefariki dunia katika mkasa mkubwa wa moto uliotokea katika kiwanda cha kutengeneza nguo katika mji mkubwa zaidi nchini Pakistan, Karachi. Mamia kadhaa ya watu waliruka kutoka paa la jengo hilo wakijaribu kujiokoa lakini wengi wakiwemo wanawake na watoto walinaswa katika jengo hilo lenye ghorofa nyingi.

Karibu magari arobaini ya wazima moto yalipambana na moto huo usiku kucha. Walioshuhudia moto huo mkubwa, walielezea kuona watu wakining'inia katika madirisha ya ghorofa za juu na kisha kuruka chini wakijaribu kujiokoa. Afisa mmoja mkuu nchini humo alisema kuwa madirisha yalikuwa yamefungwa kwa vyuma na kiwanda hicho hakikuwa na vyumba salama vya kutorokea wakati moto ukizuka.

No comments: