Wednesday, September 12, 2012

Rais mpya wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud , amenusurika jaribio la kumuua mjini Mogadishu.


Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud


Milipuko miwili imetokea nje la lango la makao ya rais huyo katika hoteli ya Al-Jazeera wakati rais huyo alipokuwa anajiandaa kufanya mkutano na waandishi wa habari.

Taarifa zinasema kuwa waziri wa mambo ya nje wa Kenya Sam Ongeri pia alikuwa katika hoteli hiyo wakati wa shambulizi. Hata hivyo wawili hao wamenusurika. Inaarifiwa mtu mmoja ameuawa.
Habari zaidi tutawaletea baadaye.

No comments: